Breaking News

Wafanyakazi wa Afrika mashariki


Wafanyakazi wa kiwanda cha korosha Mtwara

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Wafanyakazi wa kiwanda cha korosha Mtwara

Mataifa mengi hivi sasa duniani kama vile Marekani, Uingereza, Rwanda, Ujerumani, Ufaransa na nyingineza yameweza kuandaa mikakati ya kuweza kuwasaidia wafanyakzi wao.

Lakini unaweza kuona kwa nchi kama Tanzania, Kenya , Uganda na nchi nyingine za kiafrika hazijaweka bayana namna zililivyojipanga kuboresha maslahi ya wafanyakazi.

Ni vyema kufanya hivyo hivi sasa kwani gharama za maisha zimeongezeka na hivyo kupelekea hali ngumu ya kimaisha kwa watumishi wengi wa umma.

Wafanyakazi ni nyenzo muhimu sana katika taifa lolote lile kuweza kupiga hatua za kimaendeleo, kwa namna hiyo ni vyema mataifa yote kama vile Tanzania, Kenya, Uganda na nchi nyingine kuona namna ya kuboresha maslahi au mishahara ya wafanyakazi wao serikalini kwani kutasidia kuongeza ufanisi katika maeneo yao ya kazi.

Kama maslahi ya wanasiasa yalivyoboreshwa ni vyema na maslahi ya wafanyakazi wa umma nayo yakaboreshwa ili kuwewza kuendana na hali za kiuchumi zilizopo hivi sasa.

No comments