Breaking News

Wabunge waliofukuzwa Chadema wapo kwenye mikono salama - Spika Ndugai



 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Job Ndugai amesema hakuna mahali anapobanwa kwamba ni lini awafukuze wabunge 19 waliofukuzwa uanachama Chadema, katika bunge hilo.

Kauli ya Spika Ndugai imekuja wakati kukiwa na shinikizo kutoka kwa viongozi na makada wa Chadema wakimtaka Rais Samia Suluhu Hassan kuingilia kati kwa kuhakikisha wabunge hao wanaondolewa, kwani kuwepo kwao bungeni ni kinyume cha Katiba.

Wabunge hao wakiongozwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema, Halima Mdee walifukuzwa uanachama wa Chadema Novemba 27, 2020 baada kwenda bungeni kuapishwa kuchukua nafasi za viti maalum bila idhini ya chama hicho.

No comments