Hamas wafyatua zaidi ya maroketi 200 kulipiza kisasi cha shambulizi la Gaza
Wanamgambo wa Hamas wa Palestina wamesema leo kwamba wamefyatua zaidi ya maroketi 200 kuelekea nchini Israel, ikiwa ni hatua ya kulipiza kisasi cha mashambulizi kwenye jengo refu katika eneo la Ukanda wa Gaza.
Kundi hilo lililojihami kwa silaha limesema kwenye taarifa yake kwamba lilikuwa likijiandaa kufyatua makombora mengine 110 kuelekea mji wa Tel Aviv na 100 katika mji wa Beersheva, ili kulipiza kisasi cha mashambulizi yaliyoanzishwa na Israel kwenye makazi ya raia.
Hayo yanafanyika wakati waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akitangaza hali ya dharura katika jiji la Lod, wakati polisi ikiwatuhumu wakazi wa Palestina kwa kusababisha kusambaa kwa machafuko.
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa, hii leo litafanya kikao cha dharura kuujadili mzozo huo, na mjumbe wa Mashariki ya Kati kwenye umoja huo Tor Wennesland anatarajiwa kuwaarifu wanachama kuhusiana na hali ilivyo.
No comments