Breaking News

Donge nono la wanasiasa

 


Wanasiasa wameonekana kuwa na misharahara mikubwa kwa nchi za Afrika hasa Afrika ya Mashariki lakini watendaji wengi wa serikalini kama vile walimu, wauguzi, madaktari na wengine wakiwa na mishahara ya tia maji tia maji huku watu kama wabunge na mawaziri wakiwa na mishahara mikubwa, posho kubwa na viinua mgongo vikubwa jambo ambalo limetengeneza tabaka na wivu mkubwa sana katika viwango vya mishahara huku watu wengi wakitamani kuingia kwenye siasa kuliko kuwa mfanyakazi katika ofisi za umma.

Kumekuwa na tatizo la mishahara duni katika nchi za Afrika kiasi kwamba watu wanakimbia kufanya kazi kutoka serikalini na kwenda sekta binafsi na hata kuingia kwenye siasa.

Uganda

Mwaka 2017 nchini Uganda madaktari wa hospitali za umma nchini waligoma kupinga mishahara duni na uhaba wa vitendea kazi, hali iliyopelekea baadhi ya wagonjwa kufariki, hali iliyopelekea hasira nyingi za wananchi dhidi ya Serikali.

Jambo hili lilidhihirika pia Tanzania siku za karibuni pale madaktari na wauguzi walipochaguliwa na Serikali kwenda kufanya kazi katika hospitali za umma kuziacha kazi hizo na kwenda hospitali binafsi ambapo Raisi wa wakati ule Dkt. John Magufuli alitishia kuwafutia leseni zao za udaktari.

Virusi vya Corona

Hivi sasa dunia inapita kwenye wimbi zito la ugonjwa wa Corona (COVID-19) jambo ambalo limesababisha mataifa mengi duniani kuyumba kiuchumi.

Hali za wafanyakazi kwa ujumla siyo njema hata kidogo kwani gharama za maisha zimeongezeka huku mishahara yao ikibaki kuwa ile ile jambo linalowapelekea kushindwa kumudu gharama za maisha na kufanya maisha yao kuwa magumu.


Wafanyakazi wengi leo Mei 1, 2021 wanajiuliza maswali lukuki juu ya uongozi mpya wa Rais Samia Suluhu Hassan juu ya hatma ya wafanyakazi watanzania. Wanajiuliza maswali magumu;-

•Je, ataboresha maslahi (mishahara) yetu au atashikilia mpini wa Raisi aliyepita?

•Je,suala la kupandishwa madaraja kwa watumishi wa umma atalisemea vipi au mtaji wa maskini utasalia kuwa nguvu zake mwenyewe?

•Je, Mazingira ya ufanyajikazi wa watumishi wa Serikali atayatizama upya hususani vitisho vinavyotolewa na viongozi wa kiserikali dhidi ya watendaji wa serikali na ofisi nyingine za umma?

Haya ni baadhi ya machache wafanyakzi wanajiuliza juu ya siku ya wafanyakazi duniani 1 Mei, 2021 chini ya uongozi mpya wa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

No comments